Mnamo mwaka wa 1963 serikali ya Kenya aliahidi elimu ya msingi ya bure kwa watu wake. Ahadi hii haikufanikishwa hadi 2003. Wananchi wanatarajiwa kuchangia mfuko wa elimu kwa kulipia ada, kodi, na huduma za ajira. Baada ya kuchangia, wazazi wengi hawakuwa na pesa za kulipia elimu ya watoto wao na hatimaye waliachwa nje ya mfumo wa shule.
Walimu hushiriki mgomo mara nyingi kutokana na kutolipwa kwa mishahara yao. Walimu walihusika na kukusanya ada ya malipo kutoka kwa mwanafunzi, huku mishahara yao kushikiliwa hadi ada zote zilipokusanywa. Watoto wengi walikuwa wanalazimika kuacha shule tu kwa sababu hawakuweza kumudu gharama hii. Walimu mara nyingi walikuwa wakiwatuma watoto nyumbani wakati wa mitihani ya mwisho ili iwe shinikizo kwa wazazi kulipa ada ya shule.
Kwa sasa elimu ni bure, mahudhurio yameongezeka na kuna uhaba wa walimu na madarasa na watoto kutopata makini kutokana na ukosefu wa walimu wa kutosha inayotokana na msongamano wa wanafunzi madarasani. Hii ni matokeo ya watoto wote wanaohudhuria ambao hapo mwanzo hawakuweza kumudu ada ya shule, na watoto wanaotolewa shule za kibinafsi zenye hadhi ya chini ili kujinufaisha na ya elimu ya bure. Hii imejenga mahitaji kwa shule za kibinafsi zenya gharama ya chini ambazo wazazi wanaweweza kumudu kulipa ada kuwatutuma watoto wao ili kujifunza katika mazingira yaliyo bora.
Baadhi ya watu wanaamini kwamba msongamano katika mashule ni changamoto kwmba pana haja ya kuandaa mafunzo ya kiufundi zaidi ili kujenga njia mbadala kwa ajira.
Kenya ilianzisha mfumo wa sasa wa 8-4-4 mnamo mwaka wa 1985. Hii ina maana kwamba darasa la kwanza hadi la nane ni katika shule ya msingi, darasa la hadi kumi na mbili katika sekondari(Kidato cha kwanza hadi nne), na kisha wahitimu kutumia miaka minne katika chuo kikuu. Mfumo wa 8-4-4 iliundwa kusaidia wale wanafunzi ambao hawana mpango wa kuendeleza elimu ya juu. Umesaidia kupunguza viwango vya wanafunzi wanaoacha shule na kuwasaidia wale wanaoachia shule za msingi kupata ajira.
Ukuaji wa sekta ya elimu nchini Kenya umezidi matarajio. Baada ya chuo kikuu cha kwanza kuanzishwa mnamo mwaka wa 1970, vingine vitano vilitengenezwa. Mahitaji ya elimu ya juu imesababisha kuanzishwa kwa vyuo vikuu vya kibinafsi.
Vifaa katika baadhi ya vyuo vikuu vya umma ni ya hali ya chini hivi kwamba wale wa miaka ya juu hutumwa nyumbani kwa muda ili kuwapa nafasi wanafunzi wageni wanapojiunga na chuo kikuu. Vyuo vikuu, kama shule za msingi, vina ukosefu wa fedha ambazo zinazohitajika. Kuna ukosefu wa tarakilishi ya mafunzo, na maaabara ni ndogo na hazina vifaa vya kutosha. Baadhi ya wanafunzi huamua kulipa gharama ya juu kidogo ili kujiunga na vyuo vikuu vya kibinafsi kwa sababu hawataki kujihusisha na ushindani wa kutafuta nafasi za kujiandikisha. Pia, vyuo vikuu vya kibinafsi huwa na vifaa bora na maabara ya tarakilishi ya hali ya juu.
Serikali ya Uingereza inaipatia Kenya msaada wa shilingi bilioni saba (Dola milioni tisini na saba za Marekani) kusaidia kuboresha mfumo wa elimu ya bure. Fedha za ziada zitatumika kuboresha mipango ya afya katika shule zote. Pia, zitatumika katika ununuzi wa vitabu vya kusomea. Fedha hizi zitakwenda pia kupanua elimu ya shule ya upili na vyuo vikuu. Pia kutakuwa na ujenzi wa madarasa na uboreshaji wa vifaa vya ya maji pamoja na usafi wa mazingira.
Ingawa Kenya ina vyuo vikuu yake, baadhi ya wazazi huchagua kupeleka watoto wao katika nchi mbalimbali za kigeni. Wengi wanaamini kwamba Uingereza ina vyuo vikuu bora, na kwamba itakuwa fursa kubwa kwa watoto wao kuhudhuria chuo kikuu huko. Vyuo vikuu vya Kenya pia ni vigumu zaidi kujiunga navyo kutokana na mahitaji makubwa sana ya elimu ya juu na kuwepo kwa nafasi chache kwa wanafunzi kujiunga navyo.
Serikali ya Kenya ingawa kwa mwendo wa kobe, inajizatiti kufanya elimu nchini Kenya kuwa bora zadi. Miaka kumi na miwili ya kwanza ya shule sasa yanatolewa bure, japo hii ina imechangia suala la msongamano mashuleni; jambo linalohitaji kushughulikiwa kwa haraka. Ufadhili kutoka Uingereza utasaidia kujenga upya baadhi ya shule na hii itachangia kuboresha mazingira ya kujifunza.
No comments:
Post a Comment