Walimu Tanzania ni kundi huru lenye lengo la kuwaweka pamoja walimu nchini, kutoa elimu, taarifa zinazohusu au kuathiri sekta ya elimu, kukosoa, kupongeza, kujadili, na hatimaye kuwa jukwaa huru zaidi ya yaliyopo mpaka sasa. Imethibitika kuwa Serikali, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (MOEVT), Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Maafisa Elimu Madaraja ya Uteuzi na Chama Walimu Tanzania (CWT), wanashirikiana kudidimiza sekta ya walimu hususani walimu kulingana na mapunngufu mengi yaliyopo ambayo yanatuweka nyuma ya maendeleo ya dunia katika elimu.
Tunaamini kuwa changamoto zinazotukabili katika kufanikisha kuundwa kwa taasisi, mabalaza, mikusanyiko na mikakati madhubuti na endelevu ya kutoa elimu kwa walimu na jamii katika kuwania mabadiliko ya kweli ni nyingi sana. Weledi wetu unatuwezesha kupata ufahamu zaidi, kufanya mipango zaidi, kuchanganua harakati zetu zaidi, kujirtekebisha mapena tutakapokosea na hatimaye kuwa na majukwaa huru kutoka katika jamvi hili adhimu.
Kwa kuwa sekta ya elimu inajengwa na watu wenye uwezo wa kuleta mabadiliko katika sekta nyingine zote nchini. Miongoni mwa ale wanaridhika na mwenendo wa viongozi walio juu yetu kimamlaka ni wanaopokea mishahara minono, posho kubwa na kutumia rasilimali zinazotokana na kodi za wananchi ikiwamo magari. Wengine wanaoingia katika kundi hili la wachache ni walimu wasiojua haki zao kisheria, waoga, wanafiki, na wasiohitaji mabadiliko ya kweli. Mabadiliko yanayozuiwa kupatikana kutokana na ushabiki wao, upenzi wao na kuwasujudia viongozi wao wanaowatisha mithiri ya watoto wadogo na waliopoteza mika mingi katika taasisi mbalimbali za elimu walizopitia kwa kukariri.
Kwa kutumia uzoefu wa masuala yaliyoangamiza, kusambaratisha au kutokomeza kabisa makundi, asasi, na makusanyiko mengine mbalimbali. Walimu Tanzania itasimama imara dhidi ya kiongozi, muwakilishi au mshikadau yeyote atakayethubutu kutumia itikadi za udini, ukabila, ukanda, uchama wa chama chochote cha siasa, undugu, unafiki, au kusudio lolote la siri au bayana kuvuruga kusanyiko hili. Wote tunatambua kuwa kila mtu yupo huru kwa kuishi anavyopenda kwa mujibu wa vitabu vitabu vitakatifu vya Mwenyezi Mungu, Misingi ya Kitamaduni, Sheria za kimataifa na za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au kadiri mja anavyokubali kuwa ni misingi sahihi kutawala maisha yake. Hivyo uanzishaji na kuchangia mada, ushauri, kukosoa kwa ushahidi, kuelimisha au kuboresha mikakati, mipango, mbinu za kufanikisha maazimio mbalimbali, utendaji kwa ujumla uakisi lengo kuu la kuwaunganisha walimu katika kupambana na changamoto zinazoikabili sekata ya elimu. Wataalamu wengine pia wana haki ya kushirikishwa lakini iwe katika kufanikisha harakati hizi ambazo kamwe hazitofutika kwa vitisho, husda, au uharamu wowote.
Nitoe rai kwa wadau wote sasa kuongeza nguvu maradufu kuongeza wadau wengine zaidi lakini pia wasisahau kutoa utambulisho mfupi kwa kila mdau wanayewania kumpa nafasi ya kujumuika nasi katika kundi.
Ahsanteni kwa ushirikiano,
Lukinga,A (kwa niaba ya)
Ficky, M. na
Mkoba, A."
Tunaamini kuwa changamoto zinazotukabili katika kufanikisha kuundwa kwa taasisi, mabalaza, mikusanyiko na mikakati madhubuti na endelevu ya kutoa elimu kwa walimu na jamii katika kuwania mabadiliko ya kweli ni nyingi sana. Weledi wetu unatuwezesha kupata ufahamu zaidi, kufanya mipango zaidi, kuchanganua harakati zetu zaidi, kujirtekebisha mapena tutakapokosea na hatimaye kuwa na majukwaa huru kutoka katika jamvi hili adhimu.
Kwa kuwa sekta ya elimu inajengwa na watu wenye uwezo wa kuleta mabadiliko katika sekta nyingine zote nchini. Miongoni mwa ale wanaridhika na mwenendo wa viongozi walio juu yetu kimamlaka ni wanaopokea mishahara minono, posho kubwa na kutumia rasilimali zinazotokana na kodi za wananchi ikiwamo magari. Wengine wanaoingia katika kundi hili la wachache ni walimu wasiojua haki zao kisheria, waoga, wanafiki, na wasiohitaji mabadiliko ya kweli. Mabadiliko yanayozuiwa kupatikana kutokana na ushabiki wao, upenzi wao na kuwasujudia viongozi wao wanaowatisha mithiri ya watoto wadogo na waliopoteza mika mingi katika taasisi mbalimbali za elimu walizopitia kwa kukariri.
Kwa kutumia uzoefu wa masuala yaliyoangamiza, kusambaratisha au kutokomeza kabisa makundi, asasi, na makusanyiko mengine mbalimbali. Walimu Tanzania itasimama imara dhidi ya kiongozi, muwakilishi au mshikadau yeyote atakayethubutu kutumia itikadi za udini, ukabila, ukanda, uchama wa chama chochote cha siasa, undugu, unafiki, au kusudio lolote la siri au bayana kuvuruga kusanyiko hili. Wote tunatambua kuwa kila mtu yupo huru kwa kuishi anavyopenda kwa mujibu wa vitabu vitabu vitakatifu vya Mwenyezi Mungu, Misingi ya Kitamaduni, Sheria za kimataifa na za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au kadiri mja anavyokubali kuwa ni misingi sahihi kutawala maisha yake. Hivyo uanzishaji na kuchangia mada, ushauri, kukosoa kwa ushahidi, kuelimisha au kuboresha mikakati, mipango, mbinu za kufanikisha maazimio mbalimbali, utendaji kwa ujumla uakisi lengo kuu la kuwaunganisha walimu katika kupambana na changamoto zinazoikabili sekata ya elimu. Wataalamu wengine pia wana haki ya kushirikishwa lakini iwe katika kufanikisha harakati hizi ambazo kamwe hazitofutika kwa vitisho, husda, au uharamu wowote.
Nitoe rai kwa wadau wote sasa kuongeza nguvu maradufu kuongeza wadau wengine zaidi lakini pia wasisahau kutoa utambulisho mfupi kwa kila mdau wanayewania kumpa nafasi ya kujumuika nasi katika kundi.
Ahsanteni kwa ushirikiano,
Lukinga,A (kwa niaba ya)
Ficky, M. na
Mkoba, A."
No comments:
Post a Comment