Friday, February 10, 2012

''WALIMU WAPYA MANISPAA YA KINONDONI TUNATESEKA''

SISI walimu kutoka mikoa mbalimbali ya hapa nchini, tuliopangwa kufanya kazi katika manispaa ya Kinondoni mpaka sasa hatujalipwa fedha zetu za kujikimu.

 Tangu tumefika hapa Februari Mosi, hatujapewa fedha zozote, hatuna pa kulala, wala pa kula, ukizingatia kuwa wengine hatuna ndugu hapa jijini.

Kwa mfano hivi majuzi baada ya kufika hapa Manispaa ili watupe posho zetu wanatuambia hawafanyi kazi walijua ni siku kuu ya Maulid. Kweli wanakosa huruma kiasi hiki wakati sisi tungali katika maisha magumu.

 Hawajui tunaishi wapi, tunakula nini wala tunapata usafiri kwa njia gani.
Tunaomba serikali itusaidie, kama kweli wanamthamini mwalimu, basi watuokoe katika jahazi hili la tabu.

Tunataka tulipwe posho zetu zote, kama ambavyo walimu wengine walikuwa wakilipwa.

Walimu Wapya,
 Manispaa ya Kinondoni,
Dar es Salaam.

MWANANCHI

No comments: